Wednesday, October 8, 2014


 Raisi wa serekali ya mapinduzi  znz akiwasili eneo la msikitini
 Jana alasiri ilikuwa safari ya mwisho kwa Bi kidude baada ya kumaliza
swala na kumpumzisha
kwenye makazi yake ya milele......maelfu ya wananchi wakubwa
kwa watoto walifurika sana
kwenye mazishi ya kikongwe huyu alietutoka ghafla 17april majira
ya saa 7 mchana kwa saa za afrika
ya mashariki.....Viongozi wengi wa nchini walijumuika na familia
katika maziko ya Bi kidude pamoja hata na
wasanii pia walikuwepo kuonesha mchango wao.....
Zifuatazo ni picha wakati maiti ikiswaliwa Mskitini na safari ya kuelekea makaburini kwa maziko

 Rais wa Jamhuri ya mungano wa Tanzania Dk Jakaya na
Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi ndugu
Ali Mohamed Shein wakiwasili makaburini kwa ajili ya maziko

Pamoja na yote hayo ila kuna jambo mi nadhani halipo sawa kwani ni ukweli ulio wazi kuwa tunajua jinsi bi kidude alivyokuwa anaumwa na hata maisha yake binafsi yalivyokuwa ya kawaida kama sio ya shida tena magumu tofauti na kazi yake ilivyokuwa,mtakumbuka ilifikia hatua bibi huyu akazushiwa kifo yote hiyo ni kutokana na kuzidiwa kwake

Kwangu na muita bi kidude ni simba wa muziki wa taarabu na mwamba imara uliotikisa na kuitangaza tanzania njee ya nchi kwa kiasi kikubwa sana lakini kwa bahati mbaya kafa akiwa maskini,neno hili kafa akiwa maski ni neno ambalo linapendwa sana katika misiba ya wasanii nadhani tunakumbuka kwa mzee kipara kwa tx mosh wiliam,steven kanumba,sharo milioner,sajuki,mariamu muimbaji wa taarabu na wengine wengi waliotangulia mbele ya haki ndilo neno kubwa kwao.





Lakini kitu cha kujiuliza mbona hakuna mabadiliko kama tumeshajua kuwa wasanii ni maskini?mimi labda sijui mtanisaidia wadau sijawahi kusikia msanii wanchi kama uganda kenya moroco sauth africa,nigeria ghana au kwa wenzetu ulaya kafa alafu watu au serekali yao ikatangaza msanii huyu kafa maskini sijui labda kama nyie mmesikia,ila hapa kwetu ni jambo la kawaida kusemwa msanii flani kafa maskini.

 

Tuesday, October 7, 2014

Kura ya hapana: Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar atimuliwa


Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amemtimua kazi Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar (AG), Othman Masoud Othman.
Hatua hiyo ya Dk Shein imekuja ikiwa ni wiki moja tangu mwanasheria huyo kukataa ibara 22 za Katiba inayopendekezwa wakati wa Bunge Maalumu la Katiba, mjini Dodoma.
Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Dk Abdulhamid Yahya Mzee imesema Rais Shein amempandisha cheo aliyekuwa Naibu Mwanasheria Mkuu, Said Hassan Said kuwa AG.
“Amefanya mabadiliko hayo kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kupitia Ibara ya 55(1), 53, 54(1) na 55(3)... Rais Shein ametumia Sheria ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2011, Kifungu cha 12(3) na 27,” ilisema taarifa hiyo.
Othman ambaye hivi karibuni alijiondoa katika Kamati ya Uandishi ya lililokuwa Bunge Maalumu kwa kutoridhika na baadhi ya mambo, alieleza bungeni kutokubaliana na ibara ya pili, tisa, 86, 37, 70 hadi 75 na Sura ya 11 ambayo ina ibara ya 158 hadi 161, Sura ya 16 yenye ibara za 243 hadi 251 na Nyongeza ya Kwanza inayozungumzia mambo ya Muungano.
Hatua hiyo ilionekana kuwaudhi baadhi ya wajumbe ambao walimzomea na baada ya Bunge kuahirishwa, alitolewa kupitia mlango wa nyuma wa Ukumbi wa Bunge chini ya ulinzi mkali.
Baadaye Othman alisema kwamba licha ya kuwa yeye ni Mwanasheria Mkuu wa SMZ, alitumia utashi wake wa kidemokrasia kupiga kura kuzikataa ibara hizo, kutokana na kutoridhishwa na jinsi zilivyoandikwa.
“Katika suala la Katiba, Serikali ilishatamka kwenye Baraza la Wawakilishi na hata nje ya Baraza kwamba haina msimamo. Ndiyo maana uliona misimamo ilikuwa imeachwa kwenye vyama vya siasa, mimi siyo Mwanasheria Mkuu wa chama chochote.
“Kwa hiyo kama Serikali haikuwa na msimamo kwa maana ya upande… nilipiga kura kwa kuzingatia utashi wangu na maoni yangu.”


Ibara alizozikataa
Ibara ya 2. Hii inazungumzia eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, likiwamo la Tanzania Bara na la Zanzibar pamoja na madaraka ya rais wa Jamhuri kugawa eneo lolote la nchi katika mikoa.
Ibara ya 9 inayoeleza ukuu wa Katiba yenyewe na kuwa ndiyo sheria kuu. Inazuia kutungwa kwa sheria yoyote inayotofautiana nayo na inaelekeza wananchi na taasisi zote kuitii.
Sura ya Saba (Ibara 70-75). Hizi zinahusu muundo wa muungano na mgawanyo wa majukumu na mamlaka ya Serikali za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na SMZ.
Pia ibara hizo zinafafanua wajibu wa viongozi wakuu katika kuhakikisha kuwa wanatetea, wanalinda, wanaimarisha na kudumisha umoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ibara ya 86 na 87 inayofafanua utaratibu wa uchaguzi wa rais wa Muungano na taratibu za kisheria kwa mgombea asiyeridhika na matokeo ya uchaguzi mkuu kupinga uchaguzi huo mahakamani.
Ibara ya 128. Hii inahusu mamlaka ya Bunge la Muungano na Baraza la Wawakilishi katika kutunga sheria na kuzuia Baraza la Wawakilishi kutunga sheria juu ya jambo lolote ambalo liko chini ya mamlaka ya Bunge na kulizuia Bunge kutunga sheria kuhusu jambo lililoko chini ya Baraza la Wawakilishi.
Ibara za 159, 160, 161 zinazozungumzia Rais wa Zanzibar na majukumu yake, Baraza la Mapinduzi Zanzibar na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar pamoja na majukumu yake.
Sura ya 16 (243-251). Hizo zinahusu Mfuko Mkuu wa Hazina na Fedha za Jamhuri ya Muungano. Misingi ya matumizi ya fedha za umma, misingi inayoongoza matumizi ya fedha za Muungano, akaunti ya fedha ya pamoja, mfuko wa hazina na masharti ya kutoa fedha za matumizi katika mfuko huo.
Pia sura hiyo inaweka utaratibu wa kuidhinisha matumizi ya fedha kabla ya sheria inayohusu matumizi ya fedha ya Serikali, mfuko wa matumizi ya dharura na ulipaji wa mishahara ya baadhi ya watumishi.
Nyongeza ya Kwanza. Hii ni orodha ya mambo ya Muungano ambayo yameongezwa kutoka saba ya Rasimu ya Warioba kuwa 14.

Mwanasheria Mkuu mpya wa Zanzibar, Mhe Said Hassan Said

Monday, October 6, 2014

JWTZ yamtimua kazi askari

Jeshi wa Wananchi Tanzania (JWTZ) kikosi cha nchi kavu, limemfukuza kazi askari wake wa Kikosi 128 KJ cha Nyandoto, baada ya kudaiwa kuhusika katika tukio la kurushiana risasi na Polisi wa Kituo cha Stendi, wilayani Tarime.
Mbali na hatua hiyo, pia JWTZ imelaani kitendo hicho na kutaka hatua zaidi za kisheria zichukuliwe dhidi ya mwanajeshi huyo kutokana na kukiuka taratibu za kazi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Nchi Kavu, Bregedia Jenerali Mathew Sukambi alisema askari huyo ambaye hata hivyo hakumtaja jina, alisema amekiuka kiapo cha jeshi, hivyo hastahili kuwa askari tena.
“Naomba niseme, askari huyu aliyeshiriki kwenye tukio hilo lililotokea Oktoba 3, hastahili tena kuwa askari wa JWTZ, kwani amekiuka kiapo cha jeshi,” alisema Sukambi na kuongeza: “Taratibu za jeshi zinaagiza kuwa watiifu na nidhamu ya hali ya juu, hivyo kwa kitendo chake ni wazi siyo mtiifu.”
Alisema wananchi watambue kuwa jeshi halikumtuma askari huyo kufanya kitendo hicho na kwamba amekifanya yeye binafsi.
Bregedia Jenerali Sukambi aliagiza sheria zichukuliwe dhidi ya askari huyo sambamba na wote alioshirikina nao.
Tukio hilo la kurushiana rasasi na askari polisi, lilitokea Oktoba 3 mwaka huu, wilayani Tarime na kusababisha watu 12 kujeruhiwa. Sababu ya mtafaruku huo ni baada ya wanajeshi kujaribu kumchukua mwenzao aliyekamatwa na trafiki kwa kosa la kundesha pikipiki bila kuvaa kofia ngumu.

Wednesday, August 20, 2014

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mamunyange Azinduwa Uwanja wa Michezo ya Majeshi Zanzibar.



Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange, akikata utepe kuashiria kuufunguauwanja mpya wa michezo ya majeshi Zanzibar yanayotarajiwa kufunguliwa kesho na Rais waZanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein, katika uwanja wa Amaan, jumla ya nchi tano zinashiriki michezo hiyo Tanzania, Kenya, Uganda Ruwanda na Burundi.kushoto Mkuu wa Wilaya ya Mjini Magharibi Mhe.Abdallah Mwinyi Khamis na kulia Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar Shariff Shekh  Othman.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Davis Mwamunyange, akiwa na Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar Shariff Shekh Othman kulia na kushoto Mkuu wa Wilaya ya Mjini wakimshindikiza Mkuu wa Majeshi kukagua timu baada ya ufunguzi wa uwanja huo wa michezo ya Majeshi Migombani Zanzibar.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamungyange, akiikagua timu ya Vikosi vya SMZ, baada ya Kuuzindua Uwanja Mpya wa Michezo ya Majeshi, yanayotarajiwa kufunguliwa kesho uwanja wa Amaan na Rais wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein,
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamungyange, akiikagua timu ya JWTZ, baada ya Kuuzindua Uwanja Mpya wa Michezo ya Majeshi, yanayotarajiwa kufunguliwa kesho uwanja wa Amaan na Rais wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein,
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mamwunyange, akifuatilia mchezo wa kirafii kati ya JWTZ na Timu ya Vikosi vya SMZ, timu hizo zinashiriki michezo hiyo inayotarajiwa kufunguliwa kesho uwanja wa Amaan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein.

Tuesday, August 2, 2011

Mafanikio yangu mwa 2011

Ilikuwa ngumu kufikia kule ninapotaka kufika ,lakini jitihada yangu pamoja na wazazi wangu   kwa ukarimu wao waliouonesha kwangu pale nilipokuwa nasoma  masoma yangu ya web na graphic, sasa nashukuru wale wote wlionifanikisha kufikia huko walimu wangu wote wa chuo cha zanzibits na zanzicode ,kwa kupata kile ambacho nilichokuwa  nataka, Mnamo  July 7 2011 nilifanya mtihani   na kubahatika kupata cheti  cha W3school   http://www.refsnesdata.no/certification/w3certified.asp?id=2843037
WELCOME TO SEEISSAI BLOG