KIJAMII


RAISI KIKWETE AFUNGUA BARABARA YA MWENGE TEGETA


 Muonekano wa Barabara ya Mwenge Tegeta.

 Rais Jakaya Kikwete aka na Balozi wa Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaki Okada katika hafla ya uzinduzi barabara hiyo.
 Rais Jakaya Kiwete akiwa na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaki Okada pamoja na viongozi wengine wakikata utepe kuzindua barabara ya Mwenge -Tegeta.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaki Okada leo wamezindua barabara ya Mwenge Tegeta yenye urefu wa kilomita 12.9.
Uzinduzi wa barabara hiyo umefanyika katika eneo la Lugalo Mwenge jijini Dares salaam.Ujenzi na upanuzi wa barabara ya Mwenge-Tegeta ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Tanzania wa kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam.

Rais Jakaya Kikwete na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Masaki Okada wakizundua barabara hiyo.
 ________________________________________________________________________________________

KABURI LA MTOTO SHAABAN MAULID ALIYEFARIKI KISHA KUONEKANA AKIWA HAI ZAIDI YA MIAKA MIWILI ILIYOPITA LAFUKULIWA KWA AJILI YA UCHUNGUZI

SIKU chache baada kulipotiwa tukio la mtoto Shaban Maulid (15) anayedaiwa kufariki miaka miwili iliyopita na kuonekana tena akiwa hai, hivi karibuni,kaburi lake anakodaiwa kuzikwa sasa lafukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalam wa DNA

Tukio la kufukua kaburi hilo lilifanyika Jana 03.10.213 majira saa 08:30 asubuhi na kusababisha shughuli za kawaida katika mji wa Geita na mitaa yake kusimama kwa muda kwa ajili ya wakazi wa maeneo hayo kwenda kushuhudia tukio hilo lililostaajabisha wengi.

Ilipofika majira ya saa moja na nusu asubuhi watu walianza kumiminika nyumbani kwa baba wa mtoto aliyefariki kisha kuonekana na ilipofika majira ya saa mbili maofisa wa jeshi la polisi Mkoani hapa wakiambatana na mtaalamu kutoka ofisi ya mkemia mkuu kanda ya ziwa waliwasili eneo hilo.

Aidha zoezi hilo lilifanyika kwa amani baada ya askari polisi waliovalia sare na makachero kuimarisha ulinzi eneo hilo ambapo mamia ya wakazi wa Geita mjini na wale wa maeneo ya jirani kufurika eneo hilo kushuhudia tukio zima.

Akizungumza mara baada ya kufukua mabaki hayo mkemia huyo kutoka ofisi ya Kanda Lucas Ndunguru alisema wamechukua mifupa miwili mirefu kutoka kwenye miguu yote miwili kwa ajili ya kwenda kupima ili kupata ukweli halisi .

Mtaalamu huyo alisema lengo ni kutaka kujua mtoto aliyepatika kama ndiye mtoto wao halisi pamoja na kujua kilichokuwa ndani ya kaburi hilo,ambapo alisema tayari wazazi wote wamechukuliwa vipimo vya DNA kwa ajili ya kupate ukweli halisi huku akisema wanatarajia baada ya wiki mbili watakuwa wamepata majibu .

"tunakwenda kuchunguza sasa,tayari wazazi wote tumeshachukua vipimo vyao na vile vya mtoto,hatua inayofuata ni kuchunguza na hii mifupa tuliyoichukua kwa ajili ya kulinganisha na baada ya hapo ukweli utapatikana" alisema Lucas

Hata hivyo wakati wakiendelea kufukua kaburi hilo walipofika urefu wa futi moja na nusu walikutana na chungu ambacho ndani yake kulikuwa na mifupa ilisadikiwa kuwa ni ya kuku na kuleta mshangao mkubwa kwa watu .

Mtoto huyo Maulidi Shaban alionekana amefariki ndani ya kisima cha maji Tarehe 01.01.2011 baada kwenda kuchunga Mbuzi kisha kushindwa kurudi nyumbani na baadaye kuonekana baada ya siku tatu akiwa amefia kwenye kisima.

Septemba 30 mwaka huu.mtoto huyo alikutana ana kwa ana na mama yake mzazi Aziza Ramadhan wakati maeneo ya maeneo ya mtaa Mwembeni akitambuliwa kwa kila kitu na wazazi wake hata majirani na walimu wa mtoto huyo wote wakisema ni yeye bila kutia shaka.

Mtoto huyo aliyekuwa akisoma darasa la tano mwaka huo kwa sasa hajaweza kuongea vizuri ambapo kwa mujibu wa daktari wa hospitali ya wilaya Dr.Adamu Sijaona alisema mtoto huyo ataendelea kuwepo hospitalini hapo kwa uchunguzi zaidi wa kiafya ambapo alisema anaendelea vizuri.

Ofisi ya Polisi Mkoani Geita ambayo inafuatilia tukio hili kwa karibu hapa imeendelea kuwaomba wananchi kuendelea kusubiri majibu ya Mkemia mkuu ambapo wananchi hao walitaka kupata majibu siku ya Jana ya kufukua kaburi hilo





_______________________________________________________________________________________

MAJOZI MAKUBWA ZANZIBAR BAADA YA MELI KUZAMA KATIKA MKONDO WA NUNGWI








Raisi wa ZANZIBAR na mwenyekiti wa barala la mapinduzi Dk Ally Mohamed Shein wakiw ana huzuni nzito baada ya kuwasili sehemuya tukio la ajali ya meli ya Mv spice  mapema leo

__________________________________________________________________________________

MAZISHI YA SHEKHA NASOR BACHU
Inna lillahi wa inna ilaihi rajiun!
Kwa taarifa za kuaminika hii leo zinaeleza kuwa sheikh Nassor Bachu amefariki hii leo. Sheikh alianza kuugua ghafla kwa kupata stroke na baadaye kuendelea kujiuguza nyumbani kwake huku akizuiwa kudarsisha chochote kutokana na hali yake kiafya. Kwa kipindi cha kama mwaka hivi hali yake ilizidi kuwa mbaya na kubakia kuuguzwa kitandani tu na hivyo akapelekwa India mwishoni mwa mwaka 2012 kwa matibabu na kuelezewa kuwa ana mgando wa damu ndani ya ubongo wake. Tiba haikuwepo kwa hali hiyo na hivyo kurejeshwa nchini na kuendelea na dawa za kawaida.
Sheikh aliwahi kuzushiwa kifo sio chini ya mara tatu na kusababisha mwanawe kuanza kutoa taarifa katika vyombo vya habari ikiwemo redio imani kuwa ni habari za uzushi na wala familia haijapata kuomba msaada wa mchango wa matibabu.
Maziko yatakuwa kesho (14/02/2013) saa nne asubuhi Chukwani (wanawake), kusaliwa ni Masjid Sunna Kikwajuni na kuzikwa Donge – Unguja  inshallah.
MOLA AMSAMEHE MADHAMBI YAKE, AMJAALIE KAULU THABIT NA AMLAZE MAHALA PEMA PEPONI.





_________________________________________________________________________________________
RAIS DKT. KIKWETE ASIMIKWA UCHIFU WA KABILA LA WABENA MKOANI NJOMBE


 Rais Jakaya Kikwete akipokea Mkuki wakati akisimikwa Uchifu wa Kabila la Wabena na mmoja wa wawakilishi wa Wazee wa Kabila hilo,kwenye wa Hafla ya Uzinduzi wa Mkoa wa Mpya wa Njombe.

 Chifu Mpya wa Kabila la Wabena, Rais Jakaya Kikwete akiwahutubia wakazi wa Mkoa Mpya wa Njombe.



________________________________________________________________________________________
Zanzibar is a combination of two islands.Thise is Unguja and north of unguja there Pemba, it people who live in these island is approximately is one million which are 97% are Muslim, 3%Christian and other pagans
Due to with that approximately we see that most of people who live in this are Muslim and in case of Muslim in Zanzibar are divided in to two party these are :-

A)    Shia these are all Muslim who believe that there one god but they don’t believe same  calypso like Sayyid Aboubakari, Sayyid na Omar  and they believe Sayyid na Ally
B)    Sunni these are all who believe that there one god and Muhammad is prophet of Allah but they believe all calypsos.

  Due with that all party live with love each other with out make the joke another due the tradition it has
In case Christian also were divided it two type. Such as:-     
   A) catholic
   B) Pagan

In party of that Zanzibar was famous country in case religion and political in the word. in party of donation Zanzibar it was famous county which help people who got the problem of disease f    such as north America , Tanganyika 

And in case of problem of Muslim Zanzibar was the famous country which help people who was get the problem that the different country has got the solution of their problem which has same of them are Uganda ,Kenya ,Sudan, and other

Also Zanzibar was the center of business in east Africa due to his condition it has and the different country has desire to established the business in these islands and also the thing make famous in the word was the first county to has the taa za barabarani with was use the light gas.


In party of revolution Zanzibar it has got in January 12, 1964 from the last sultan sayyid na baraghash and after introduce the multiparty system in 1992 Zanzibar has lost it quality from other word after happed conflict of same party. The different agreement happen but nothing thing has change  and the different diplomatic people they came but  no one can make good.
                            
                               





Hon Amani karume talk with maalim Sefu and
Dr Ali moh'd sheni in ed-el-fitri day


____________________________________________________________________________________
MABOMU NDANI YA DARAJANI
Watu wasiofahamika bado, usiku wa kuamkia jana Jumatatu walitupa kitu kinachosadikiwa kuwa bomu lililokuwa katika mfano wa 'sausage' karibu na eneo la biashara kando ya Barabara ya Darajani mjini Zanzibar.

Msaidizi wa Kamishna wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar Mkadam Khamis Mkadam akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana kuhusu taarifa hiyo alisema, mlinzi binafsi, Amour Kassim Amour (36), aliyekuwa kazini kwenye Duka la Sahara, aliona idadi ya watu katika gari aina ya 'pickup' wakitokea Bwawani kuelekea Mkunazini, walikwenda uelekeo wa dukani alipokuwa akilinda, na walipofika hapo walipunguza mwendo, ndipo mmoja wao aliporusha guruneti upande wake, na kitu hicho kilitua katikati ya masanduku yaliyokuwa mbele ya duka hilo.

"lilikuwa likitoa moshi. Kwa ushujaa, Amour aliliokota na kulitupa mbali na maduka," "Kwa bahati, Amour alilitupa kwenye uwanja wa wazi na hakukuwa na wanunuzi katika mtaa huo wenye shughuli nyingi kwa sababu ilikuwa ni usiku," alisema Mkadam akiongeza kwamba guruneti lililipuka kwa mlipuko wenye sauti kubwa dakika chache baadaye.

Polisi walifanikiwa kupata mabaki ya unga unga na kukusanya kokoto zilizotokana na athari ya mlipuko huo.

Polisi wameanzisha msako na uchunguzi katika tukio hilo, na kuwataka Wazanzibari kuwa watulivu na kuripoti kitu chochote kinachoshukiwa

No comments:

WELCOME TO SEEISSAI BLOG