Wednesday, October 8, 2014


 Raisi wa serekali ya mapinduzi  znz akiwasili eneo la msikitini
 Jana alasiri ilikuwa safari ya mwisho kwa Bi kidude baada ya kumaliza
swala na kumpumzisha
kwenye makazi yake ya milele......maelfu ya wananchi wakubwa
kwa watoto walifurika sana
kwenye mazishi ya kikongwe huyu alietutoka ghafla 17april majira
ya saa 7 mchana kwa saa za afrika
ya mashariki.....Viongozi wengi wa nchini walijumuika na familia
katika maziko ya Bi kidude pamoja hata na
wasanii pia walikuwepo kuonesha mchango wao.....
Zifuatazo ni picha wakati maiti ikiswaliwa Mskitini na safari ya kuelekea makaburini kwa maziko

 Rais wa Jamhuri ya mungano wa Tanzania Dk Jakaya na
Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi ndugu
Ali Mohamed Shein wakiwasili makaburini kwa ajili ya maziko

Pamoja na yote hayo ila kuna jambo mi nadhani halipo sawa kwani ni ukweli ulio wazi kuwa tunajua jinsi bi kidude alivyokuwa anaumwa na hata maisha yake binafsi yalivyokuwa ya kawaida kama sio ya shida tena magumu tofauti na kazi yake ilivyokuwa,mtakumbuka ilifikia hatua bibi huyu akazushiwa kifo yote hiyo ni kutokana na kuzidiwa kwake

Kwangu na muita bi kidude ni simba wa muziki wa taarabu na mwamba imara uliotikisa na kuitangaza tanzania njee ya nchi kwa kiasi kikubwa sana lakini kwa bahati mbaya kafa akiwa maskini,neno hili kafa akiwa maski ni neno ambalo linapendwa sana katika misiba ya wasanii nadhani tunakumbuka kwa mzee kipara kwa tx mosh wiliam,steven kanumba,sharo milioner,sajuki,mariamu muimbaji wa taarabu na wengine wengi waliotangulia mbele ya haki ndilo neno kubwa kwao.





Lakini kitu cha kujiuliza mbona hakuna mabadiliko kama tumeshajua kuwa wasanii ni maskini?mimi labda sijui mtanisaidia wadau sijawahi kusikia msanii wanchi kama uganda kenya moroco sauth africa,nigeria ghana au kwa wenzetu ulaya kafa alafu watu au serekali yao ikatangaza msanii huyu kafa maskini sijui labda kama nyie mmesikia,ila hapa kwetu ni jambo la kawaida kusemwa msanii flani kafa maskini.

 

No comments:

WELCOME TO SEEISSAI BLOG