Jeshi wa Wananchi Tanzania (JWTZ)
kikosi cha nchi kavu, limemfukuza kazi askari wake wa Kikosi 128 KJ cha
Nyandoto, baada ya kudaiwa kuhusika katika tukio la kurushiana risasi na
Polisi wa Kituo cha Stendi, wilayani Tarime.
Mbali na hatua hiyo, pia JWTZ imelaani kitendo
hicho na kutaka hatua zaidi za kisheria zichukuliwe dhidi ya mwanajeshi
huyo kutokana na kukiuka taratibu za kazi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwa niaba
ya Mkuu wa Majeshi ya Nchi Kavu, Bregedia Jenerali Mathew Sukambi
alisema askari huyo ambaye hata hivyo hakumtaja jina, alisema amekiuka
kiapo cha jeshi, hivyo hastahili kuwa askari tena.
“Naomba niseme, askari huyu aliyeshiriki kwenye
tukio hilo lililotokea Oktoba 3, hastahili tena kuwa askari wa JWTZ,
kwani amekiuka kiapo cha jeshi,” alisema Sukambi na kuongeza: “Taratibu
za jeshi zinaagiza kuwa watiifu na nidhamu ya hali ya juu, hivyo kwa
kitendo chake ni wazi siyo mtiifu.”
Alisema wananchi watambue kuwa jeshi halikumtuma askari huyo kufanya kitendo hicho na kwamba amekifanya yeye binafsi.
Bregedia Jenerali Sukambi aliagiza sheria zichukuliwe dhidi ya askari huyo sambamba na wote alioshirikina nao.
Tukio hilo la kurushiana rasasi na askari polisi,
lilitokea Oktoba 3 mwaka huu, wilayani Tarime na kusababisha watu 12
kujeruhiwa. Sababu ya mtafaruku huo ni baada ya wanajeshi kujaribu
kumchukua mwenzao aliyekamatwa na trafiki kwa kosa la kundesha pikipiki
bila kuvaa kofia ngumu.
No comments:
Post a Comment