Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Freeman Mbowe akiwasili kwenye makao makuu ya Jeshi la Polisi
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Freeman Mbowe akiwasili
kwenye makao makuu ya Jeshi la Polisi nchini,Mapema leo asubuhi tayari
kwa kwenda kuhojiwa juu kauli aliyoitoa kwenye Mkutano Mkuu wa chama
hicho hivi katibuni,kuwa watafanya maandamano nchini nzima bila kikomo.
Siku moja baada ya makamu wa rais dkt mohamed ghalib bilal
kuhimiza mahusiano mema wakati wa utendaji kazi baina ya vyombo vya
ulinzi na usalama na vyombo vya habari, jeshi la polisi likiwa na silaha
pamoja na mbwa limekiuka kauli hiyo kwa kuwapiga na kuwajeruhi baadhi
ya waandishi wa habari na kuwazuia kutekeleza wajibu wao wakati
mwenyekiti wa Chama cha demokrasia na maendeleo Chadema alipowasili
katika makao makuu ya jeshi hilo kwa mahojiano.Kauli hiyo ya makamu wa rais imeshindwa kutekelezwa kutokana na tukio lililotokea majira ya saa 5 na dk 15 asubuhi wàkati mwenyekiti wa chadema taifa Mhe. Freeman Mbowe alipowasili makao makuu na askari wa polisi kutaka kuzuia gari alilopanda kuingia ndani ya lango kuu pamoja na waandishi wa habari na watu wengine kuamriwa kuondoka katika eneo hilo agizo lililopingwa na waandishi wa habari na baadhi ya wanasheria wa Chadema.
Kufuatia na kutolewa kwa ilani hiyo jeshi la polisi kikosi cha kutuliza ghasia-FFU- kilianza kupiga waandishi wa habari pamoja na baadhi ya wananchi huku wengine wakikimbia kuhofu vipigo toka kwa askari hao ambapo baaadhi ya waandishi walioumizwa sehemu mbalimbali ya mihili yao.
Akiwatangazia wafuasi waliokuwa wakikataa kuondoka katika maeneo hayo mwanasheria wa chadema mhe. Tundu lissu licha ya kuwahakikishia kuwa mwenyekiti wa chama hicho taifa Mhe. Freeman Mbowe yuko salama amewataka kuondoka katika eneo hilo na kurudi majumbani ili kuepusha vurugu na misongamano ambayo ingeweza kusababisha matatizo zaidi.
Aidha ITV imeshuhudia mwenyekiti wa Chadema taifa Mhe Freeman Mbowe akitoka makao makuu ya jeshi la polisi akisindikizwa na ulizni mkali wa jeshi la polisi kuelekea katika ofisi za makao makuu ya chama hicho baada ya kukamilika kwa taratibu za kipolisi
Wafuasi wa Chadema wakimsindikiza mwenyekiti wao Freeman Mbowe kuelekea Makao makuu ya jeshi la polisi
Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika akizungumza na waandishi wa
habari waliokuwepo kwenye eneo la makao makuu ya Jeshi la Polisi,juu ya
kile kilichokuwa kikiendelea kwenye mahojiani katika ya Mwenyekiti wa
Chama hicho na Jeshi
Huyu alikuwa akikaidi amri ya Jeshi la Polisi ilibidi aondolewe kwa nguvu.
Makamu
Mwenyekiti wa Chadema,Prof. Abdallah Safari na Wakili wa Chama,Wakili
Mabele Marando wakiwasili kwenye Makao Makuu wa Jeshi la Polisi.
------------------------------
------------------------------
Mapokezi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Dr Ali Mohamed Shein Unguja
Viongozi mbalimbali wachama cha Mapinduzi wakiwa katika Mapokezi ya
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM huko katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Abeid Aman Karume Zanzibar
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambae pia ni Rais wa
Zanzibar Dk,Ali Mohd Shein akisalimiana na Viongozi wa Chama hicho na Wananchi
mbalimbali waliokwenda kumpokea hapo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman
Karume Zanzibar.
Msafara wa Wapanda Pikipiki wa Chama cha Mapinduzi ukiwa mbele katika
Mapokezi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambae pia ni Rais wa
Zanzibar Dk,Ali Mohd Shein ukitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman
Karume Zanzibar.
Msafara wa Wapanda Pikipiki wa Chama cha Mapinduzi ukiwa mbele katika
Mapokezi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambae pia ni Rais wa
Zanzibar Dk,Ali Mohd Shein ukitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman
Karume Zanzibar.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambae pia ni Rais wa
Zanzibar Dk,Ali Mohd Shein akiwapungia Mkono Wananchi na Wanachama wa Chama cha
Mapinduzi akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume Zanzibar
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambae pia ni Rais wa
Zanzibar Dk,Ali Mohd Shein (watatu kulia)akijumuika na Viongozi mbalimbali wa
Dini na Chama katika Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid
Amaan Karume ili kumuombea Dua Rais huyo mara baada ya kufika katika Makao
Makuu ya Chama hicho Kisiwa Ndui Zanzibar.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambae pia ni Rais wa
Zanzibar Dk,Ali Mohd Shein akitoa hotuba kwa Wazee wa Chama cha Mapinduzi (CCM)
waliofika Mkao Makuu ya Chama ili Kumpongeza kwa kuchaguliwa kwake huko Dodoma
na kumtakia kheri katika Kuiongoza Zanzibar.
______________________________________________________________
Maandamano ya CHADEMA Mkoa wa Dodoma yamedhibitiwa kwa Mkoa mzima.Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi wa Polisi EMMANUEL G. LUKULA (ACP) (pichani) amesema katika hilo kuna gari lenye namba za usajili T.792 CAX aina ya Pick up Ford Ranger nyeupe mali ya CHADEMA iliyokuwa ikiendesha na CHRISTOPHER NYAMWINJA, Mweneye miaka 52, Mgogo, Mkristo Mratibu wa CHADEMA Kanda ya magharibi ambapo makazi yake ni TABORA mjini limekamatwa mtaa wa KUU karibu na kituo cha mafuta cha GAPCO...
CHADEMA iliyokuwa ikiendesha na CHRISTOPHER NYAMWINJA, Mweneye miaka 52, Mgogo, Mkristo Mratibu wa CHADEMA Kanda ya magharibi ambapo makazi yake ni TABORA mjini limekamatwa mtaa wa KUU karibu na kituo cha mafuta cha GAPCO jirani na WIMPI RESTAURANT likiwa na watu wengine watatu ambao ni:-
1. LAURENT S/O MANGWESHI mwenye miaka 36, Mkristo, Msukuma Mkulima wa Wialya ya Mpanda Mkoa wa Katavi.
2. AGNES D/O STEPHANO mwenye miaka 26, Mhehe, Mkristo Mfanyabiashara Mkazi Ubungo MAziwa Dar es Salaam.
3. ELISHA S/O DAUDI mwenye miaka 49, Msukuma, Mkristo Fundi umeme Mkazi wa TAbora.
Kamanda LUKULA – ACP amesema gari hilo lilikuwa na bango lenye maandishi “TUNAPINGA UFISADI UNAOFANYWA NA BUNGE LA KATIBA”. Likiwa na maandishi ubavuni mbele na nyuma M4C.
Aidha Kamanda LUKULA – ACP ameongeza kuwa kabla ya kukamatwa kwa gari hilo Polisi walilikimbiza na katika kupita kwenye kona/mtaa watu wawili waliruka kutoka kwenye gari hilo na kukimbia kusikojulikana na bango hilo. Watu waliobaki ndani ya gari hilo ambao ni wanne ndio waliokamatwa.Askari Polisi wakiwa kwenye zoezi la kuzuia Maandamano ya Chadema Mjini Dodoma
_________________________________________________________________________________________
YALIYOJIRI BUNGENI MARA BAADA YA MWANASHERIA WA SEREKALI YA ZANZIBAR KUPINGA BAZI YA VIFUNGU
______________________________________________________________
POLISI YAZIMA MAANDAMANO YA CHADEMA
Jeshi la polisi mkoani Dodoma leo limezima maandamano yaliyopangwa
kufanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupinga
kuendelea kwa vikao vya Bunge la Katiba kwa kile wanachodai ni kufuja
fedha za umma.Maandamano ya CHADEMA Mkoa wa Dodoma yamedhibitiwa kwa Mkoa mzima.Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishina Msaidizi wa Polisi EMMANUEL G. LUKULA (ACP) (pichani) amesema katika hilo kuna gari lenye namba za usajili T.792 CAX aina ya Pick up Ford Ranger nyeupe mali ya CHADEMA iliyokuwa ikiendesha na CHRISTOPHER NYAMWINJA, Mweneye miaka 52, Mgogo, Mkristo Mratibu wa CHADEMA Kanda ya magharibi ambapo makazi yake ni TABORA mjini limekamatwa mtaa wa KUU karibu na kituo cha mafuta cha GAPCO...
CHADEMA iliyokuwa ikiendesha na CHRISTOPHER NYAMWINJA, Mweneye miaka 52, Mgogo, Mkristo Mratibu wa CHADEMA Kanda ya magharibi ambapo makazi yake ni TABORA mjini limekamatwa mtaa wa KUU karibu na kituo cha mafuta cha GAPCO jirani na WIMPI RESTAURANT likiwa na watu wengine watatu ambao ni:-
1. LAURENT S/O MANGWESHI mwenye miaka 36, Mkristo, Msukuma Mkulima wa Wialya ya Mpanda Mkoa wa Katavi.
2. AGNES D/O STEPHANO mwenye miaka 26, Mhehe, Mkristo Mfanyabiashara Mkazi Ubungo MAziwa Dar es Salaam.
3. ELISHA S/O DAUDI mwenye miaka 49, Msukuma, Mkristo Fundi umeme Mkazi wa TAbora.
Kamanda LUKULA – ACP amesema gari hilo lilikuwa na bango lenye maandishi “TUNAPINGA UFISADI UNAOFANYWA NA BUNGE LA KATIBA”. Likiwa na maandishi ubavuni mbele na nyuma M4C.
Aidha Kamanda LUKULA – ACP ameongeza kuwa kabla ya kukamatwa kwa gari hilo Polisi walilikimbiza na katika kupita kwenye kona/mtaa watu wawili waliruka kutoka kwenye gari hilo na kukimbia kusikojulikana na bango hilo. Watu waliobaki ndani ya gari hilo ambao ni wanne ndio waliokamatwa.Askari Polisi wakiwa kwenye zoezi la kuzuia Maandamano ya Chadema Mjini Dodoma
_________________________________________________________________________________________
YALIYOJIRI BUNGENI MARA BAADA YA MWANASHERIA WA SEREKALI YA ZANZIBAR KUPINGA BAZI YA VIFUNGU
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar,
Mhe. Othman Masoud Othman akipiga kura leo kwenye ukumbi wa Bunge Maalum
la Katiba mjini Dodoma kupitisha Sura na Ibara za Rasimu ya Katiba
inayopendekezwa
Mjumbe wa Bunge Maalum la
Katiba, Mhe. Yahya Kassim Issa akiomba mwongozo leo Bungeni kwa
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta kuhusu kitendo
cha Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman kuja kupiga
kura na kukataa baadhi ya Ibara za Rasimu ya Katiba inayopendekezwa
wakati alijitoa kwenye Kamati ya Uandishi ambapo alitakiwa awepo
akitetea maslahi ya Zanzibar, jambo ambalo limewachanganya baadhi ya
wajumbe
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar,
Mhe. Othman Masoud Othman akisindikizwa kutoka ndani ya ukumbi wa Bunge
Maalum leo mjini Dodoma na Askari Polisi
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar,
Mhe. Othman Masoud Othman (mwenye Kaunda suti ya kijivu) akisindikizwa
kutoka nje ya viwanja vya Bunge Maalum la Katiba leo mjini Dodoma na
Askari Polisi mara baada ya kushutumiwa na baadhi ya Wajumbe wa
Zanzibar.
No comments:
Post a Comment